TEHRAN (IQNA)- Sherehe inayojulikana kama Naqqareh Zani imefanyika katika Haram Takatifu ya Imam Ridha AS, katika mji wa Mashhad, kaskazini mashariki mwa Iran katika mkesha wa kukumbuka kuzaliwa Imamu huyo wa Nane wa Madhehebu ya Shia.
Naqqareh ni aina Fulani ya ngoma ya nchi za Asia Magharibi na hutumika wakati wa sherehe za Haram ya Imam Ridha AS.
Tarehe 11 Dhulqaada mwaka ni siku ya kukumbuka kuzaliwa Imam Ali bin Mussa Ridha AS, mmoja kati ya Watu wa Nyumba ya Mtume Muhammad SAW. Mwaka huu, siku hii inasadifiana na Juni 22.