Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Mauritania, misikiti hiyo iliyopokea misaada iko katika mkoa wa Adrar, kaskazini mwa nchi hiyo ya kaskazini magharibi mwa Afrika.
Nakala hizo za Qur'ani zimesambazwa na Idara ya Masuala ya Kiislamu na Elimu mkoani humo kwa ushirikiano na Jumuiya ya Maimamu wa Sala ya Ijumaa Mauritania.
Katika miaka ya hivi karibuni, majengo mengi, ikiwemo misikiti, imeharibika kutokana na mafuriko katika katika maeneo kadhaa ya Mauritania hasa mkoa wa Adrar.
Misikiti mingi iliyoharibiwa katika mafuriko imekarabatiwa upya na sasa inatumika. Jamhuri ya Kiislamu ya Mauritania ina idadi ya watu milioni 4 ambao karibu wote ni Waislamu.