Filamu ya "Ardhi Yangu" (My Land) inayozungumzia ardhi ya Palestina ambayo imetengezwa na Nabil Ayouch itaonyeshwa katika jumba la michezo ya kuigiza la Chuo cha Utafiti wa Sayansi za Jamii mjini Paris, Ufaransa.
2011 Mar 05 , 21:05
Silisila ya vikao vya kuchunguza maisha ya Mtume Muhammad (saw) na historia ya Uislamu vitaanza tarehe 11 Mchi mjini Paris, Ufaransa.
2011 Mar 05 , 14:59
Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sanaa za Kiislamu cha Tabriz (magharibi mwa Iran) akiwa pamoja na wasaidizi, wanachama wa jopo la kielimu, wakuu wa vitengo mbalimbali na wasanii wa chuo hicho mapema leo wamekutana na Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Ali Khamenei. Katika mkutano huo kumezinduliwa Qur'ani yenye thamani kubwa iliyofumwa juu ya zulia.
2011 Mar 05 , 10:04
Kongamano la "Mtume Muhammad (saw), Kigezo Bora kwa Ajili ya Mashariki na Magharibi" limepangwa kufanyika tarehe 26 Machi chini ya usimamizi wa Kituo cha Semina za Sayansi za Kiislamu cha Cambridge (CISS) nchini Uingereza.
2011 Mar 02 , 20:08
Rais Christian Wulff wa Ujerumani akiandamana na mkewe pamoja na ujumbe wake rasmi ametembelea jumba la mambo ya kale ya sanaa ya Kiislamu mjini Doha Qatar.
2011 Mar 02 , 16:07
Warsha ya elimu ya maana ya zaka kwa watoto wadogo wa Ufaransa imeanza leo katika kituo cha Kiislamu cha Tauhidi katika mji wa Lyon.
2011 Feb 28 , 17:42
Maonyesho ya kaligrafia ya Kiislamu na Kiarabu imeanza leo Jumatatu mjini Jeddah Saudi Arabia kwa udhamini wa Taasisi ya Utafiti, Utamaduni, Sanaa na Historia ya Kiislamu IRCICA.
2011 Feb 28 , 16:23
Maonyesho ya sayansi na ubunifu katika ulimwengu wa Kiislamu yanayojumuisha athari za maandiko ya kielimu na kisayansi ya Waislamu yanafanyika katika jumba la makumbusho la mji mkuu wa Malaysia, Kuala Lumpur.
2011 Feb 27 , 16:12
Waziri wa Wakfu na Masuala ya Kidini wa Algeria ametangaza habari ya kushiriki wanafunzi wa shule za msingi, sekondari na wanachuo 40,000 katika mashindano ya mtandao wa intaneti yaliyopewa jina la 'kumetemtea Mtume (saw)'.
2011 Feb 24 , 12:11
Kamati ya Taifa ya Haki za Binadamu ya Qatar (NHRC) ikishirikiana na Kituo cha Kiislamu na Kiutamaduni cha Qatar (Fanar) vimechapisha kitabu kilichopewa jina la Uislamu na Haki za Binadamu.
2011 Feb 23 , 15:13
Sherehe za kuadhimishwa kuzaliwa Mtume Mtukufu (saw) zimepangwa kufanyika leo Jumapili katika Kituo cha Kiislamu cha London, Uingereza.
2011 Feb 20 , 17:51
Gazeti la Habari za Waislamu limeanza kuchapishwa nchini Ghana kwa mnasaba wa maadhimisho ya ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran.
2011 Feb 16 , 18:05
Kundi la kiutamaduni la al-Fatimiyaat la mjini al-Awamiya katika mkoa wenye wakazi wengi wa Kishia wa Qatif limeandaa tamasha la Sera za Mtume (saw) maalumu kwa wanawake wa Kishia wa Saudi Arabia kwa mnasaba wa kusherehekea Maulidi ya Mtume Mtukufu (saw).
2011 Feb 16 , 16:05