IQNA

Shughuli za Qur'ani

Misri yazindua kozi za kimataifa za Qur'ani Tukufu kwa njia ya mtandao

20:40 - June 11, 2023
Habari ID: 3477134
Wizara ya Wakfu ya Misri imezindua kozi tatu za mtandaoni za Qur'ani kwa wanafunzi kutoka nchi mbalimbali.

Wizara hiyo ilisema washirikki 85 kutoka nchi za mabara tofauti wamechukua kozi hizo. Wanatoka Urusi, Marekani, Ufaransa, Ujerumani, Nigeria, Kongo, na Ivory Coast miongoni mwa wengine. Wanapokea masomo juu ya kusoma na kuhifadhi Qur'ani Tukufu, fikra za Qur'ani, tovuti ya Akhbar al-Yawm iliripoti.
Wale watakaofaulu vyema masomo hayo watapata vyeti vya kuhifadhi robo ya Quran Tukufu. Kutumia mtandao kwa ajili ya kufundisha Qur'ani na kutoa kozi za Qur'ani mtandaoni kumeendelezwa katika miaka ya hivi karibuni kwani huwapa watu kote ulimwenguni fursa ya kujifunza Qur'ani Tukufu   Nchini Misri, wizara ya Awqaf ina jukumu la kuandaa, kuratibu na kusimamia shughuli za Qur'ani na kidini.
 
4146218

captcha