Viongozi wa Saudia wamewaomba viongozi wa misafara mbalimbali ya Kiislamu nchini humo kushiriki kwenye shughuli ya kuwazika mahujaji wengi walioaga dunia huko Mina Alhamisi iliyopita, ambao wameshindwa kutambuliwa na jamaa zao, ambao idadi yao kwa uchache ni watu mia sita. Imearifiwa kuwa miili ya mahujaji walioaga dunia imeharibika na kuna wasiwasi juu ya uwezekano wa kutokea mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu. Aidha upigaji picha mahujaji waliokufa umepigwa marufuku na kwamba viwiliwili vya wahanga hao vinatazamiwa kuzikwa katika makaburi ya umati. Utawala wa Aal Saud umechukua hatua hiyo huku misafara mingi ya nchi za Kiislamu ikibanisha wasiwasi wao baada ya kutoweka idadi kubwa ya mahujaji wao kwenye maafa ya Mina.../mh