IQNA

Dola 5,000 Hutumika Kugharramia Mazishi ya Mwislamu Marekani

12:16 - May 24, 2016
Habari ID: 3470331
Waislamu wa Marekani hawakabiliwi na matatizo katika kipindi cha uhai wao tu bali hata wanapofariki dunia matatizo hayo bado huwaandama.

Hayo yameelezwa na Ibrahim Hooper Mkurugenzi wa Baraza la Mahusiano ya Kiislamu la Marekani ambaye amebainisha kwamba, Waislamu wanaoishi Marekani wanalalamikia gharama kubwa za mazishi na hatua ya viongozi wa nchi hiyo ya kutotoa ushirikiano kwa ajili ya kuzikwa Waislamu kwa mujibu wa sheria za Kiislamu.

Inaelezwa kuwa, kwa kiwango cha wastani gharama za mazishi ya Mwislamu hugharimu kiasi cha dola elfu tano nchini Marekani. Mkurugenzi wa Baraza la Mahusiano ya Kiislamu nchini Marekani amesema kuwa, tangu mwaka 2011 Waislamu wamekuwa wakitaka watengewe na serikali makaburi maalumu ya Waislamu mjini New York ili Waislamu wa mji huo wasilazimike kuwazika maiti wao katika jimbo la New Jersey, lakini hadi sasa hakuna hatua yoyote iliyochukuliwa na serikali kutekeleza ombi hilo.

Kwa mujibu wa Baraza la Mahusiano ya Kiislamu la Marekani ni kuwa, Waislamu hugharamika mno katika suala la mazishi hasa gharama za usafiri kutokana na kulazimika kusafirisha maiti wao masafa ya mbali kwa ajili ya kwenda kuzika kutokana na kuwa maeneo wanayoishi hakuna makaburi ya Waislamu.

3500154

captcha