Katika mazungumzo ya simu nyakati tafauti, Haniya na Nakhala wameelekeza matumaini yao kuwa Raeisi atafanikiwa katika kipindi chake cha urais. Aidha wameishukuru Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kwa kuunga mkono harakati za ukombozi wa Palestina.
Haniya ametoa ufafanuzi kuhusu ushindi wa hivi karibuni wa harakati za ukombozi wa Palestina dhidi ya utawala wa Kizayuni huku akisisitiza kuhusu kuimarishwa uhusiano baina ya Hamas na Iran.
Naye rais mteule wa Iran wamewapongeza watu wa Palestina kwa ushindi wao huku akisisitiza kuwa Jamhuri ya Kiislamu itaendelea kuunga mkono ukombozi wa Quds (Jerusalem). Aidha Raeisi amelaani vikali kuendelezwa mzingiro dhidi ya Ukanda wa Ghaza.