IQNA

Semina ya ‘Hatari ya Fikra ya Kitakfiri’ kufanyika Misri

8:58 - February 16, 2014
Habari ID: 1375500
Wizara ya Awqaf na Masuala ya Kidini nchini Misri imeandaa semina yenye anuani ya ‘Hatari ya Fikra za Kitakfri’.

Kwa mujibu wa Shirika la Kimataifa la Habari za Qur'ani IQNA, Waziri wa Awqaf Misri Sheikh Mohammad Mokhtar  Gomaa amesema semina hiyo itafanyika Jumanne wiki hii na kuwashirikisha maimamu wa misikiti kutoka maeneo yote ya Misri. Viongozi hao wa Kiislamu watachunguza hatari kubwa ya fikra za kitakfiri ambazo zinaenezwa na wafuasi wa pote la Kiwahabi. Sheikh Mohammad Mokhtar  Gomaa amesema wizara yake pia inapanga kuandaa semina 100 katika misikit na vituo vya vijana kote Misri kwa lengo la kubainisha kuhusu hatari ya fikra za kitakfiri katika jamii ya Waislamu. Ameongeza kuwa Misri inahitaji kwa uchache miaka mitano kukabiliana na hatari  matakfiri au watu wenye misimamo mikali wanaowakufurisha Waislamu. Aidha amesema watu wasio na utaalamu wa masuala ya Uislamu hawataruhusiwa kutoa hotuba katika misikiti nchini humo. Hivi karibuni Sheikh Nabil Qauq, Naibu Mwenyekiti wa Baraza la Utendaji la Harakati ya Hizbullah nchini Lebanon alionya kuhusu njama za magaidi wa Kiwahabi nchini humo na kusema: "Ugaidi wa kitakfiri hauna dini na wala si dhehebu bali ni shari kamili na ni shari mutlaki na ni tishio kwa watu wote."

1375373

Kishikizo: awqaf gomaa takfiri
captcha